Mchezo huo ambao utapigwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa saa moja usiku tunategemea utakuwa mgumu kutokana na ubora wa wapinzani wetu.
Wachezaji wameshiriki mazoezi hayo kikamilifu na wamejitahidi kuonyesha uwezo mkubwa ili kulishawishi benchi la ufundi kuwapa nafasi ya kucheza kesho.
Advertisement
Tunaiheshimu Ihefu lakini tumejiandaa kuhakikisha tunashinda ili kuendelea kubaki katika nafasi za juu kwenye msimamo.