Simba Sports Club
News

Timu yafanya mazoezi ya mwisho kujiandaa na Ihefu

27 Oct 2023

Mchezo huo ambao utapigwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa saa moja usiku tunategemea utakuwa mgumu kutokana na ubora wa wapinzani wetu.

Wachezaji wameshiriki mazoezi hayo kikamilifu na wamejitahidi kuonyesha uwezo mkubwa ili kulishawishi benchi la ufundi kuwapa nafasi ya kucheza kesho.

Advertisement

Tunaiheshimu Ihefu lakini tumejiandaa kuhakikisha tunashinda ili kuendelea kubaki katika nafasi za juu kwenye msimamo.

Back to homepage
Share this story