Kama ulivyokuwa mchezo wa jana dhidi ya Al Dhafrah mechi ya kesho pia itapigwa katika Mji wa Abu Dhabi hivyo kikosi kitaondoka Dubai mchana.
Kocha Mkuu Roberto Oliviera 'Robertinho' amesema anaridhishwa na jinsi wachezaji wanavyopokea mafunzo yake ambapo ana matumaini makubwa ya kufanya vizuri kikosi kitakaporejea Dar es Salaam.