Simba Sports Club
News

Timu yafanya mazoezi ya mwisho kujiandaa na Al Dhafrah

12 Jan 2023

Kikosi kitaondoka kesho kuelekea Abu Dhabi ambako mchezo huo utafanyika na wachezaji wote wameshiriki mazoezi ya mwisho.

Katika hatua nyingine, Kocha Mkuu Roberto Oliviera 'Robertinho' amefurahishwa na jinsi wachezaji wanavyojituma na kushika vizuri mafunzo anayowapa.

Advertisement

Morali ya wachezaji ipo juu wanafanya jitihada mazoezini ili kumshawishi Kocha Robertinho awape nafasi.

Aidha, mshambuliaji Moses Phiri naye ameanza mazoezi mepesi baada ya kupona majeraha yake yaliyomfanya kukosa mechi mbili za mwisho za ligi.

Back to homepage
Share this story