Wachezaji wote isipokuwa Joshua Mutale na Ayoub Lakred ambao ni majeruhi wameshiriki mazoezi hayo na wapo tayari kwa mchezo wa kesho.
Katika mazoezi hayo yaliyoongozwa na Kocha Mkuu Fadlu Davids na wasaidizi wake hakuna mchezaji aliyepata maumivu ambayo yanaweza kumfanya kuukosa mchezo wa kesho.