Simba Sports Club
News

Timu yafanya mazoezi ya mwisho Gymkhana

18 Dec 2023

Wachezaji wote wameshiriki kikamilifu na morali ipo juu kuhakikisha tunashinda na kufufua matumaini ya kutinga hatua ya robo fainali.

Ushindi katika mchezo wa kesho utakuwa ni wa kwanza kwenye hatua hii ndio maana tumejipanga kuhakikisha tunashinda.

Advertisement

Haitakuwa mechi rahisi kutokana na ubora wa Wydad lakini tupo imara kupambana hadi mwisho ili kuwapa furaha Wanasimba na kubaki na alama tatu nyumbani.

Katika mchezo huo tutakosa huduma ya nyota wetu Saido Ntibazonkiza na Sadio Kanoute ambao wanatumikia adhabu ya kadi tatu za njano.

Back to homepage
Share this story