Kanuni za CAF zinataka timu mgeni kufanya mazoezi katika Uwanja utakaotumika siku moja kabla ya mchezo lakini kutokana na kesho dimba hilo litakuwa na matumizi mengine hivyo tumetakiwa kufanya mazoezi leo.
Wachezaji wote 23 ambao tumesafiri nao kwa ajili ya mchezo huo wameshiriki mazoezi hayo na hakuna yoyote ambaye amepata maumivu ambayo yanaweza kumfanya kuukosa mchezo wa Ijumaa.
Advertisement
Pamoja na kujua tuna kibarua kigumu kucheza na timu bora ugenini tukiwa nyuma kwa bao moja lakini wachezaji wana morali kubwa na matumaini ya kufuzu hatua ya nusu fainali ni makubwa.