Simba Sports Club
News

Timu yafanya mazoezi Tanga kabla ya kuanza safari ya kurejea Dar

10 Mar 2024

Jana tuliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Coastal Union kwahiyo wachezaji walitakiwa kufanya mazoezi ya utimamu ili kujiweka sawa kutokana na ratiba kubana.

Saa nane mchana kikosi kitaanza safari ya kurejea Dar es Salaam tayari kwa maandalizi ya mchezo wa Jumanne dhidi ya Singida Fountain Gate.

Advertisement

Kesho kikosi kitaendelea na program ya mazoezi kwa ajili ya mchezo wa Jumanne ambao utapigwa katika Uwanja wa Azam Complex Chamazi.

Back to homepage
Share this story