Kikosi kilitakiwa kufanya mazoezi hayo kesho kwenye uwanja huo kwa mujibu wa kanuni lakini imeshindikana kutokana na muda huo kuwa na mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika.
Wachezaji wote 22 tuliosafiri nao wameshiriki mazoezi hayo na wapo kamili kuipigania timu kupata pointi tatu.
Advertisement
Kesho kikosi kitafanya mazoezi ya mwisho kujiweka sawa kabla ya Jumapili saa moja usiku kwa saa Tanzania kushuka katika Uwanja wa Novemba 11 kuikabili Bravos.