Tunauchukulia kwa umuhimu mkubwa mchezo wa kesho na tutaingia kwa tahadhari huku tukiwaheshimu TRA lengo likiwa kuhakikisha tunashinda na kutinga hatua ya 16 bora.
Tunawaomba mashabiki kujitokeza kwa wingi uwanjani kesho katika mchezo huo kwa ajili ya kuipa sapoti timu ili tufanikishe malengo ya kutinga katika hatua hiyo.