Kikosi kimefanya mazoezi asubuhi katika Uwanja wa Mao Tse Tung kujiandaa na mchezo wa Nusu Fainali ya Michuano ya Mapinduzi utakaopigwa Jumatatu.
Mechi kati ya Azam FC na Namungo ambao wanamalizia mechi zao za makundi ndiyo itaamua timu ya kucheza nayo ambapo atakayemaliza nafasi ya pili ndiyo tutakutana naye nusu fainali.
Advertisement
Wachezaji wote wamefanya mazoezi na hakuna aliyepata majeruhi katika mchezo wetu wa jana dhidi ya Mlandege.
Wachezaji wameendelea kuonyesha uwezo mkubwa mazoezini ili kulivutia benchi la ufundi kwa ajili ya kutaka kupewa nafasi kwenye mchezo wa nusu fainali.