Simba Sports Club
News

Timu yaendelea na mazoezi Visiwani Zanzibar

17 Apr 2025

Kikosi kimewasili jana hapa Zanzibar tayari kwa mchezo huo ambao malengo yetu ni kuhakikisha tunapata ushindi mzuri nyumbani ili kujiweka kwenye hali nzuri katika mechi ya marudiano ugenini.

Wachezaji wote wameshiriki mazoezi hayo kikamilifu na morali zao zipo juu na wanaonekana wapo tayari ajili ya kuipambania timu kufikia malengo tuliyojiwekea.

Advertisement

Kikosi kitaendelea na programu ya mazoezi kesho na keshokutwa kabla ya kushuka dimbani siku ya Jumapili.

Back to homepage
Share this story