Kikosi kimewasili jana hapa Zanzibar tayari kwa mchezo huo ambao malengo yetu ni kuhakikisha tunapata ushindi mzuri nyumbani ili kujiweka kwenye hali nzuri katika mechi ya marudiano ugenini.
Wachezaji wote wameshiriki mazoezi hayo kikamilifu na morali zao zipo juu na wanaonekana wapo tayari ajili ya kuipambania timu kufikia malengo tuliyojiwekea.
Advertisement
Kikosi kitaendelea na programu ya mazoezi kesho na keshokutwa kabla ya kushuka dimbani siku ya Jumapili.