Mazoezi hayo yamesimamiwa na kocha mkuu Roberto Oliveira 'Robertinho' akisaidiana na wasaidizi wake wa benchi la ufundi.
Mchezaji pekee ambaye amekosekana kwenye mazoezi ya leo ni mlinzi wa kulia, Shomari Kapombe ambaye amepewa mapumziko ya wiki moja kutokana na kupata maumivu katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Raja Casablanca.
Advertisement
Wachezaji, Augustine Okrah, Ismael Sawadogo na Peter Banda ambao walikuwa majeruhi wote wamerejea na wameshiriki mazoezi hayo.