Simba Sports Club
News

Timu ya vijana yaichapa Ihefu Azam Complex

13 May 2024

Mchezo ulianza kwa kasi huku timu zote zikishambuliana kwa zamu huku tukilisakama zaidi lango la mpinzani na wao wakijibu mapigo kwa mashambulizi ya kushtukiza.

Pamoja na mashambulizi mengi ya pande zote lakini katika dakika 45 za kipindi cha kwanza hakuna timu iliyopata bao.

Kipindi cha pili tulianza kwa kasi na kuwashambulia Ihefu na dakika ya 63 tulipata bao la kwanza lililofungwa na Razak Bashir kwa mpira wa kona ambayo ilingia moja kwa moja wavuni

Advertisement

Dakika tano baadaye tuliendelea kuwashambulia na kuzidi kuwapa presha na kufanikiwa kupata bao la pili lililofungwa na Juma Ali.

Baada ya ushindi wa leo kikosi chetu cha vijana kitashuka tena uwanjani Jumatano katika mchezo wa pili wa kundi A.

Back to homepage
Share this story