Mchezo wetu wa kwanza utakuwa Septemba 25 dhidi ya Kipanga FC utakaopigwa Uwanja Amani na mchezo wa pili utapigwa Septemba 27 katika Uwanja huo huo wa Amani ambapo mechi zote zitachezwa saa moja usiku.
Baada ya michezo hiyo miwili timu itarejea jijini Dar es Salaam Septemba 28.
Advertisement
Tayari kikosi kimeanza mazoezi leo kufuatia mapumziko ya siku mbili waliopewa wachezaji baada ya kumaliza mchezo wa hatua ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Nyasa Big Bullets.