Simba Sports Club
News

Timu kupaa Misri Alhamisi kwa Pre Season

12 Jul 2022

Wachezaji wote ambao tutakuwa nao msimu ujao watakuwepo safarini isipokuwa wale ambao watakuwa kwenye majukumu ya timu za taifa ambao watajiunga haraka wakimaliza.

Kambi hiyo ya mwezi mmoja itakuwa katika Mji wa Ismailia ambao tunaamini utamsaidia Kocha Zoran Maki na wasaidizi wake kukiandaa kikosi.

Advertisement

Kikosi kitarejea nchini Agosti 5 na Agosti 13 tutashuka katika Uwanja wa Benjamin Mkapa kuikabili Yanga kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii kuashiria kufunguliwa kwa pazia la Ligi Kuu ya NBC.

Back to homepage
Share this story