Kikosi kitaondoka na wachezaji 22 kuelekea jijini Mbeya kikiwa kamili kwa mpambano huo ambao tunaamini utakuwa mgumu kutokana na upinzani tunaokutana nao hasa wakiwa nyumbani.
Baada ya kufika timu itafanya mazoezi ya mwisho kesho saa 10 jioni katika Uwanja wa Sokoine kujiweka tayari kwa mtanange wa Jumatano.
Advertisement
Wachezaji wote ambao wapo kwenye orodha ya safari hali yao ni nzuri tayari kuipigania timu ugenini kutafuta alama tatu.