Simba Sports Club
News

Timu kuondoka kesho kuelekea Afrika Kusini

22 Apr 2025

Kikosi kitaondoka na Ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) ambapo itapitia Johannesburg kabla ya kuunganisha kuelekea Durban ambapo ndipo kutakapopigwa mchezo huo.

Baada ya kikosi kufika Afrika Kusini kesho jioni kitafanya mazoezi ya Gym ili kuweka miili sawa kutokana na uchovu wa safari.

Advertisement

Timu inaondoka ikiwa na matumaini ya kutinga fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika licha ya ugumu ambao tunategemea kukutana nao.

Back to homepage
Share this story