Kikosi kitaondoka na jumla ya wachezaji 23 tayari kwa mchezo huo ambao tunaamini utakuwa mgumu kutokana na wapinzani wetu Mashujaa kuwa katika nafasi ambayo sio nzuri kwenye msimamo.
Katika mchezo wa jana tulioibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Tembo FC kutoka Tabora hatukupata majeruhi yoyote ambaye tutamkosa katika mechi ya Jumamosi.
Advertisement
Kikosi kitafanya mazoezi ya mwisho kesho katika Uwanja wa Lake Tanganyika kabla ya kuivaa Mashujaa Jumamosi.
Licha ya kufahamu utakuwa mchezo mgumu lakini tutaingia uwanjani kwa lengo la kuhakikisha tunashinda na kuondoka na pointi zote tatu.