Baada ya mapumziko ya siku moja waliopewa wachezaji waliporudi kutoka Angola jana walianza mazoezi na leo jioni wataingia kambini moja kwa moja.
Wachezaji wote 24 ambao tulisafiri nao kwenda Angola wapo kwenye hali nzuri na jana wamefanya mazoezi na wataingia kambini.
Advertisement
Tumejipanga kuingia katika mchezo wa Jumapili bila kuangalia matokeo mazuri ya mechi ya kwanza, hatutaki sababu yoyote itufanye tukose kufuzu hatua ya makundi.
Tayari viingilio vya mchezo vimetangazwa na vituo zinapotikana pia vimewekwa hadharani ili mashabiki wanunue mapema kuepusha usumbufu siku ya mechi.