Simba Sports Club
News

Timu kuifuata Nsingizini Hotspurs Alhamisi

14 Oct 2025

Kikosi kitaondoka na wachezaji 22 na benchi zima la ufundi kwa usafiri wa Ndege ya Air Tanzania kikipitia Afrika Kusini kabla ya kuunganisha mpaka Eswatini.

Baada ya kufika Eswatini kikosi kitakuwa na muda wa siku mbili kufanya mazoezi kabla ya Jumapili kushuka dimbani kuwakabili Nsingizini.

Advertisement

Mchezo dhidi ya Nsingizini utapigwa katika Uwanja wa Taifa wa Somhololo saa 10 jioni kwa saa za Tanzania.

Back to homepage
Share this story