Baada ya kumalizika mchezo wa jana dhidi ya Namungo FC ambao tuliibuka na ushindi wa mabao 3-0 kikosi kilirudi Mtwara kujiweka tayari kwa safari ya kurudi Dar es Salaam.
Kikosi kitakapowasili Dar es Salaam kitaingia kambini moja kwa moja kujiandaa na mchezo wa Ligi unaofuata dhidi ya Azam FC utakaopigwa Jumatatu, Februari 24 katika Uwanja wa KMC Complex.