Hii ni rekodi nyingine tunaiweka kujaza uwanja kuelekea Simba Day siku nne kabla ya tukio lenyewe.
Tiketi za Platinum ziliisha siku ya kwanza baada ya kutangazwa zikifuatiwa na VIP A kabla ya leo majukwaa mengine yote kujaa.
Zoezi la kuuza tiketi lilianza wiki moja iliyopita lakini mwamko wa Wanasimba umekuwa mkubwa na leo tumeweka rekodi nyingine.
Viingilio vilikuwa kama ifuatavyo:
Mzunguko Sh. 5000
Advertisement
Machungwa Sh. 10,000
VIP C Sh. 20,000
VIP B Sh. 30,000
VIP A Sh. 40,000
Platinum Sh. 200,000