Mchezo huo ambao utakuwa ni wa marudiano utapigwa nchini Morocco, Machi 26 kufuatia ile ya kwanza iliyopigwa jijini Dar es Salaam, Novemba 21, 2023 na Stars kupoteza kwa mabao 2-0.
Nyota hao ni mlinda mlango Ally Salim, walinzi Shomari Kapombe, Mohamed Hussein 'Zimbwe Jr' na Abdulrazak Hamza.
Advertisement
Wengine walioitwa ni pamoja na viungo Yusuph Kagoma na Kibu Denis.
Taifa Stars itaingia kambini kesho kujiandaa na mchezo huo.