Simba Sports Club
News

Simba yawasili salama jijini Mwanza

16 Apr 2021 By simbasc 1,464 views

Kikosi kimetua salama jijini Mwanza tayari kwa mechi tatu za Kanda ya Ziwa ambazo ni Mwadui FC, Kagera Sugar na Gwambina FC.

Baada ya kufika kikosi kitapumzika na kesho kitasafiri kuelekea Shinyanga kwa ajili ya mchezo dhidi ya Mwadui utakaopigwa Jumapili katika Uwanja wa Kambarage.

Advertisement

Baada ya mchezo huo kikosi kitaelekea mkoani Kagera kuifuata Kagera Sugar mchezo utakaopigwa Aprili 21 katika dimba la Kaitaba.

Tutamaliza ziara ya mikoa ya Kanda ya Ziwa Aprili 24 kwa kucheza na Gwambina FC katika Uwanja wa Gwambina.

Back to homepage
Share this story