Simba Sports Club
News

Sakho Mchezaji Bora Simba Januari

2 Feb 2022 By simbasc 1,572 views

Kiungo Mshambuliaji Pape Ousmane Sakho, amechaguliwa Mchezaji Bora wa Mashabiki wa mwezi Januari (Emirate Aluminium ACP Simba Fans Player of the Month).

Sakho raia wa Senegal amewapiku nyota wenzake wawili Sadio Kanoute na Henock Inonga ambao aliingia nao fainali.

Katika mwezi Januari Sakho amecheza mechi saba akidumu uwanjani dakika 563 na amefunga mabao matatu huku akionyesha kiwango safi.

Kwa ushindi huo Sakho atakabidhiwa fedha taslimu Sh 2,000,000 na tuzo kutoka kwa wadhamini Emirate Aluminium ACP.

Advertisement

Mchanganuo wa kura zilivyopigwa

Pape Sakho - 58.02% (1015)

Henock Inonga - 34.67% (607)

Sadio Kanoute - 7.31% (128)

Back to homepage
Share this story