Simba Sports Club
News

Sakho mchezaji bora dhidi ya Namungo

10 Jan 2022

Kiungo mshambuliaji Pape Ousmane Sakho, amechaguliwa mchezaji bora wa mchezo wetu wa Nusu Fainali ya Michuano ya Mapinduzi dhidi Namungo FC baada ya kuonyesha kiwango safi.

Licha ya kufunga bao la pili na kusababisha la kwanza lililofungwa na Medie Kagere, Sakho alikuwa mwiba mkali kwa walinzi wa Namungo kwa muda wote aliokuwa Uwanjani.

Advertisement

Pamoja na kuonyesha kandanda safi pia Sakho alikuwa anaburudisha mashabiki kwa jinsi alivyokuwa anauchezea mpira kwa madoido.

Sakho amekabidhiwa fedha taslimu Sh 1,000,000 kutoka kwa wadhamini Kampuni ya Bima ya NIC.

Back to homepage
Share this story