Phiri ambaye pia anaweza kucheza nafasi za kiungo mshambuliaji na winga zote mbili atavaa jezi nyekundu na nyeupe kuanzia msimu ujao wa mashindano.
Phiri ni usajili wetu wa kwanza kuelekea maboresho makubwa ya kikosi chetu ambayo tumepanga kuyafanya kuelekea msimu mpya unaotarajiwa kuanza mapema hivi karibuni.
Advertisement
Msimu uliopita akiwa na Zanaco Phiri amefunga mabao 14 kwenye ligi kuu ya Zambia akiwa ni mfungaji bora namba mbili nyuma ya kinara mwenye mabao 16.