Simba Sports Club
News

Rais Samia atutumia Salam za Pongezi

2 Mar 2024 By simbasc 584 views
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan ametupongeza kwa kufanikiwa kufuzu hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuichakaza bila huruma Jwaneng Galaxy kutoka Botswana kwa mabao 6-0. Rais Dkt. Samia amesema ushindi huu sio tu kwa ajili ya Simba pekee bali ni Watanzania wote. "Hongereni sana Klabu ya Simba kwa kufanikiwa kufuzu hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika. Mafanikio yenu sio furaha na fahari kwa mashabiki na wanachama wa Simba bali pia kwa Taifa na Watanzania wote," amesema Rais Dkt. Samia.
Advertisement
Back to homepage
Share this story