Simba Sports Club
News

Quuens yapangwa Kundi A Mabingwa Afrika

9 Sep 2022

Queens ambayo inawakilisha Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) imepangwa na timu za Afsa FC (Morocco), Green Buffalo (Zambia) na Determine Girls (Libya).

Hii ni mara ya kwanza ya kikosi cha Queens kushiriki michuano hiyo mikubwa Afrika kwa Wanawake ambapo pia kwa Tanzania ni timu ya kwanza kufanya hivyo.

Advertisement

Queens ilipata nafasi hiyo baada ya kuifunga SHE Corporates kutoka Uganda katika mchezo wa Fainali ya Michuano ya CECAFA iliyofanyika Uwanja wa Azam Complex mwezi uliopita.

Michuano hiyo itashirikisha timu nane kutoka barani Afrika ambazo kila moja inawakilisha ukanda wake.

Back to homepage
Share this story