Simba Sports Club
News

Queens yaingia kambini kujiandaa na Ligi ya Mabingwa

20 Sep 2022

Kikosi hicho kinachonolewa na Kocha Sebastian Nkoma kimeanza maandalizi mapema ili kuhakikishia tunakwenda kufanya vizuri kwenye michuano hiyo mikubwa barani Afrika.

Katika maandalizi hayo, leo saa 10 jioni kikosi kitafanya mazoezi katika Uwanja wa Mo Arena na baada ya hapo kitaingia kambini moja kwa moja.

Advertisement

Queens ambayo inawakilisha Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) imepangwa Kundi A pamoja na timu za Afsa FC (Morocco), Green Buffalo (Zambia) na Determine Girls (Libya).

Back to homepage
Share this story