Simba Sports Club
News

Queens yaichakaza The Tigers Arusha

10 May 2022

Mchezo ulianza kwa kasi tulishambulia lango lango la The Tigers ambapo dakika ya 20 Asha Djafar alitupatia bao la kwanza ambalo lilidumu mpaka mapumziko.

Kipindi cha pili tuliongeza kasi na kufanya mashambulizi ambapo dakika ya 60 Falone Pambani alitupatia bao la pili akimalizia mpira wa krosi uliopigwa na Asha Djafar.

Kiungo Joelle Bukuru alikamilisha karamu ya mabao kwa kufunga la tatu dakika ya 70 kwa mkwaju wa penati baada ya yeye mwenyewe kufanyiwa madhambi ndani ya 18.

Advertisement

Kocha Sebastian Nkoma aliwatoa Amina Ramadhani na Asha Djafar na kuwaingiza Olaiya Barakat pamoja na Mercy Tagoe.

Ushindi huu unatufanya kufikisha alama 54 tukiwa kileleni mwa msimamo baada ya kucheza mechi 19.

Back to homepage
Share this story