Mchezo huo ulikuwa wa upande mmoja huku Queens ikitawala karibia kila idara kuanzia mwanzo wa mchezo hadi mwisho.
Katika mchezo huo mabao yetu yalifungwa na Jentrix Shikangwa, Danai Bhobo, Shelda Boniface na Zainabu Mohamed waliofunga mawili kila mmoja.
Advertisement
Mengine yamefungwa Diakiese Kaluzodi, Silivia Mwacha, Asha Rashid, Asha Djafar, Aisha Mnuka na Olaiya Barakat.
Katika kipindi hiki ambacho Ligi Kuu ya Wanawake imesimama kikosi chetu kinaendelea na mazoezi pamoja na kucheza mechi za kirafiki.