Mchezo huo wa Nusu Fainali ambao tunatarajia utakuwa mgumu utapigwa kesho saa tano asubuhi katika Uwanja wa Abebe Bikila.
Wachezaji wote wameshiriki mazoezi hayo na hakuna aliyepata maumivu ambayo yatamfanya kuukosa mchezo huo muhimu ambao lengo letu ni kushinda ili kutinga fainali.
Advertisement
Morali za wachezaji zipo juu na kila mmoja yupo tayari kuhakikisha anaipambania timu kufikia malengo yake.