Prinil (28) raia wa Afrika Kusini atakuwa na jukumu la kuwasoma wapinzani kupitia video na kuchambua ubora na mapungufu yao na kukabidhi kwa benchi la ufundi ili kurahisha njia ya kuwakabili.
Prinil ni kijana mdogo mwenye uzoefu mkubwa ambapo amewahi kufanya kazi na Venda FC, Mamelodi Sundowns, Durban City zote za Afrika Kusini.
Advertisement
Prinil ameshatua nchini akiendelea kufuatilia taratibu za kibali cha kazi kabla ya kuanza rasmi kutekeleza majukumu yake.