Simba Sports Club
News

Pablo awamwagia sifa wachezaji

28 Nov 2021

Kocha Mkuu Pablo Franco, amewasifu wachezaji kwa kujituma muda wote wa mchezo na kutufanya kupata ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Red Arrows ya Zambia.

Pablo amesema kila mchezaji alifanya kazi yake vizuri na kutimiza majukumu uwanjani jambo ambalo limemvutia katika mchezo wa leo.

Advertisement

Hata hivyo, Pablo amesema tulikuwa na uwezo kupata mabao zaidi ya matatu tuliyopata kama wachezaji wangeongeza umakini katika nafasi tulizotengeneza.

Back to homepage
Share this story