Simba Sports Club
News

Onyango, Mzamiru, Okrah wachuana Tuzo Mchezaji Bora Oktoba

31 Oct 2022

Wachezaji hao ni mlinzi wa kati Joash Onyango, kiungo mkabaji Mzamiru Yassin na kiungo mshambuaji Augustine Okrah.

Kabla ya kuchujwa na kubaki watatu walikuwa watano wakiwemo kiungo mshambuaji, Clatous Chama na mshambuliaji Moses Phiri.

Takwimu zao za mwezi Oktoba

Mechi Dakika Assist Mabao

Joash 6 540 0 0

Advertisement

Mzamiru 5 450 1 1

Okrah 5 366 2 2

Zoezi la kupiga kura limeanza tayari kupitia tovuti yetu ya www.simbasc.co.tz na litakamilika Novemba 2 saa sita usiku kisha mshindi wa jumla atatangazwa.

Mshindi wa jumla atakabidhiwa fedha taslimu Sh milioni mbili na tuzo kutoka kwa wadhamini Wakuu Emirate Aluminium Profile.

Back to homepage
Share this story