Wachezaji watatu bado wana mkataba na tumewatoa kwa mkopo wakati mmoja tumefikia makubaliano ya pande mbili ya kuachana nae.
Wachezaji ambao tumewatoa kwa mkopo ni Shaban Idd Chilunda aliyeenda KMC, Jimmyson Mwanuke ametua Mtibwa Sugar na Mohamed Musa aliyejiunga na Kagera Sugar.
Advertisement
Kiungo mkabaji Nassor Kapama yeye amejiunga na Mtibwa Sugar kwa mkataba wa moja kwa moja kwakuwa tumefikia makubaliano ya pande mbili ya kutoendelea nae.
Aidha Uongozi wa klabu unawatakia kheri wachezaji hao katika timu zao mpya wanazokwenda.