Kwa mara nyingine tumeendelea kuonyesha tuna kikosi bora msimu huu baada ya wachezaji wetu 16 kuitwa kwenye timu zao za taifa zinazojiandaa na mechi za kufuzu Kombe la Dunia.
Awali wachezaji 17 waliitwa lakini baada ya kupata majeraha mlinzi wetu wa kulia Shomari Kapombe ameenguliwa kwenye kikosi cha Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inayojiandaa na mchezo dhidi ya Benin.
Ifuatavyo ni orodha ya wachezaji wetu walioitwa timu zao za taifa.
Tanzania (Taifa Stars)
1. Aishi Manula 2. Israel Patrick 3. Mohamed Hussein 4. Kennedy Juma 5. Jonas Mkude
6. Mzamiru Yassin 7. Erasto Nyoni 8. John Bocco 9. Kibu Denis
Malawi (The Flames)
10. Peter Banda 11. Duncan Nyoni
Zambia (Chipolopolo)
12. Rally Bwalya
Uganda (The Cranes)
13. Taddeo Lwanga
Rwanda (Amavubi)
14. Medie Kagere
Kenya (Harambee Stars)
15. Joash Onyango
DR Congo
16. Henock Inonga Baka