Simba Sports Club
News

Nyota sita waitwa Taifa Stars

20 May 2022 By simbasc 1,166 views
Wachezaji sita kutoka katika kikosi chetu wameitwaTimu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) itakayoingia kambini kujiandaa kufuzu Michuano ya AFCON mwaka 2023. Taifa Stars itacheza mechi mbili za kufuzu dhidi ya Niger pamoja na Algeria. Nyota hao walioitwa ni mlinda mlango Aishi Manula walinzi Shomari Kapombe, Mohamed Hussein na Kennedy Juma. Wengine ni kiungo Mzamiru Yassin na mshambuliaji Kibu Denis ambao watatuwakilisha katika kikosi hicho cha Stars.
Advertisement
Back to homepage
Share this story