Simba Sports Club
News

Nyota saba waitwa Taifa Stars

15 Mar 2022 By simbasc 1,375 views

Wachezaji wetu saba wameitwa katika kikosi cha Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inayojiandaa na mechi mbili za kirafiki za kimataifa zilizopo kwenye kalenda ya Shirikisho la soka Duniani (FIFA).

Taifa Stars itacheza mechi yake ya kwanza Machi 23 dhidi ya Jamhuri ya Afrika ya Kati na Sudan Machi 29 zote zikipigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Wachezaji walioitwa ni

Advertisement

Aishi Manula
Shomari Kapombe
Israel Mwenda
Mohamed Hussein
Mzamiru Yassin
Jonas Mkude
Kibu Dennis

Baada ya mchezo wetu wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya ASEC Mimosas utakaopigwa Machi 20 nchini Benin wachezaji hao wataruhisiwa kujiunga na kikosi cha Stars.

Back to homepage
Share this story