Kikosi cha wachezaji 23 kimefika salama mkoani Mara tayari kwa mchezo wetu wa kwanza wa ligi dhidi ya Biashara United utakaopigwa kesho Jumanne katika Uwanja wa Karume saa 10 jioni.
Timu iliondoka jana saa 12 kwa Ndege kuelekea jijini Mwanza kabla ya leo asubuhi kuanza safari ya kuja Mara.
Kikosi hicho hicho ndicho kitaenda kuikabili Dodoma Jiji katika mchezo wetu wa pili utakaopigwa Septemba 30, katika Uwanja wa Jamhuri jijini humo.
Kikosi Kamili kinachosafiri
Makipa
1. Ally Salim
2. Beno Kakolanya
3. Aishi Manula
Walinzi
4. Israel Patrick
5. Shomari Kapombe
6. Mohamed Hussein
7. Pascal Wawa
8. Henock Inonga Baka
9. Kennedy Juma
10. Erasto Nyoni
Viungo
11. Mzamiru Yassin
12. Rally Bwalya
13. Pape Sakho
14. Peter Banda
15. Hassan Dilunga
16. Duncan Nyoni
17. Taddeo Lwanga
18. Jimmyson Mwinuke
Washambuliaji
19. Chris Mugalu
20. John Bocco
21. Medie Kagere
22. Yusuph Mhilu
23. Kibu Denis