Simba Sports Club
News

Ntibazonkiza Mfungaji bora NBCPL

12 Jun 2023 By simbasc 232 views
Kiungo mshambuliaji, Saido Ntibazonkiza ameshinda tuzo ya mfungaji bora wa Ligi ya NBC msimu 2022/23 baada ya kufunga mabao 17. Ntibazonkiza amefunga mabao sawa na mshambuliaji wa Yanga, Fiston Mayele ambaye nae amekabidhiwa kiatu cha dhahabu. Katika msimu wa 2022/23 Ntibazonkiza amefunga mabao hayo 17 pamoja na kusaidia kupatikana kwa mengine 12. Ntibazonkiza amefunga mabao hayo akiwa na timu mbili za Simba na Geita ambapo akiwa kwetu ametupia 11.
Advertisement
Back to homepage
Share this story