Mzamiru ni miongoni mwa mihili mikubwa ya kikosi chetu na kiwango chake hakijawahi kutetereka tangu tumsajili kutoka Mtibwa Sugar miaka sita iliyopita.
Uongozi baada ya kupitia ripoti ya mwalimu umeridhishwa na kiwango cha Mzamiru na kumuongezea kandarasi mpya.
Advertisement
Kuelekea msimu mpya wa ligi 2022/23 tunaendelea kuimarisha kikosi ikiwemo kuwaongezea mikataba wachezaji ambao tunaamini bado ni msaada mkubwa kwetu.