Simba Sports Club
News

Mtoto awakilisha mashabiki nchi nzima

23 Jun 2022

Uongozi wa klabu umetumia mchezo wetu wa mwisho wa nyumbani tuliocheza na Mtibwa Sugar kuwashukuru mashabiki kwa mchango wao mkubwa waliotupa tangu mwanzo mpaka leo.

Mtendaji Mkuu wa Klabu, Barbara Gonzalez amemkabidhi mtoto Bernadetha jezi maalumu ikiwa na maana ya kuwashukuru mashabiki wote nchi nzima.

Advertisement

Kabla ya kumkabidhi Bernadetha jezi hiyo, Barbara alitembelea vikundi vyote vya hamasa vilivyojitokeza uwanjani kwenda kuwashukuru.

Baada ya kumalizika kwa mchezo Viongozi na Maafisa wa klabu walishuka chini ya uwanja na kuwapungia mashabiki kuonyesha tunawathamini.

Back to homepage
Share this story