Simba Sports Club
News

Mo awatembelea wachezaji kambini

21 Apr 2023

Mo amewakumbusha wachezaji umuhimu wa kushinda mchezo wa kesho sababu mioyo na furaha za Wanasimba zinawategemea hivyo wasiwaangushe.

Mo amewaambia mchezo utakuwa mgumu kutokana na ubora wa Wydad lakini kama watajitoa kwa asilimia 100 na uwepo wa mashabiki wetu uwanjani tutapata ushindi mzuri kesho.

Advertisement

Mo amekuwa na utaratibu wa kutembelea kambini kuzungumza na wachezaji kila tunapokaribia mechi kubwa ili kuwatia hamasa na kuwaongezea morali.

Kutokana na ukubwa na umuhimu wa mchezo Mo ameambatana na Bodi ya Wakurugenzi ili kuwasisitiza wachezaji kujitoa kuhakikisha ushindi unapatikana.

Back to homepage
Share this story