Simba Sports Club
News

Mo akutana na Viongozi wa SEN

14 Jul 2024

SEN ni mtandao wa mashabiki wa Simba ambao huchangia ada ya 1,500,000 kwa mwaka kwa ajili ya miradi maalumu ya miundombinu ya klabu.

Wanachama wa SEN hupata faida nyingi kama bima za maisha, tiketi za mechi na faida nyingine nyingi.

Advertisement

Kikao hicho kilihudhuriwa na Viongozi wa SEN akiwapo Mwenyekiti Abdulrazak Badru, Makamu wake Farouk Baghoza, Katibu Dkt. George Ruhago, Katibu Msaidizi Richard Mwalibwa na wanachama wa SEN.

Menejimenti ya Simba iliongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu, Imani Kajula

Back to homepage
Share this story