Simba Sports Club
News

Mechi dhidi ya TRA imeahirishwa

14 Mar 2026

Bodi ya Ligi ya Tanzania (TPLB) tayari imetoa taarifa rasmi juu ya kuahirishwa kwa mchezo kutokana na Uwanja kushindwa kukidhi vigezo kwa mujibu wa kanuni.

Kwa mujibu wa kanuni 34.1 (1.4) ya Ligi Kuu kuhusu kuahirisha mchezo na Kanuni ya 39:13 kuhusu waamuzi, kutokana na mvua kubwa inayoendelea kunyesha katika Jiji la Arusha uwanja Sheikh Amri Abeid haufai kwa matumizi kwa mujibu wa kanuni.

Advertisement

Tunasubiri TPLB kutoa taarifa ya kupangiwa tarehe nyingine ya mchezo huo.

Back to homepage
Share this story