Simba Sports Club
News

Mechi dhidi ya Azam kupigwa Benjamin Mkapa

22 Feb 2025

Taarifa ya TPLB imesema sababu ya kuutoa mchezo huo kutoka katika Uwanja wa KMC Complex kuupeleka Benjamin Mkapa ni kutokana na ukubwa wa mechi ambao tunategemea mashabiki watakuwa wengi.

Msimu huu tumechagua Uwanja wa KMC Complex kwa ajili ya mechi zetu za nyumbani lakini kutokana na ukubwa wa mchezo TPLB imeupeleka katika dimba la Benjamin Mkapa ambalo lina uwezo wa kuingiza mashabiki 60,000.

Maandalizi ya mchezo huo ambao tunaamini utakuwa mgumu kutokana na ubora wa Azam yanaendelea vizuri na malengo yetu ni kuhakikisha tunashinda na kuchukua alama tatu.

Viingilio vya mchezo ni kama ifuatavyo:

Advertisement

VIP A Sh. 30,000

VIP B Sh. 20,000

Machungwa Sh.10,000

Mzunguko Sh. 5,000

Back to homepage
Share this story