Simba Sports Club
News

Matola awamwagia sifa wachezaji ushindi wa Mbeya City

17 Jun 2022

Matola amesema tulijua mchezo utakuwa mgumu kutokana na ushindani tunaopata kila tukikutana na City lakini wachezaji walijitahidi kufanikisha ushindi huo.

Matola amesema kipindi cha kwanza tulicheza vizuri tukatengeneza nafasi nyingi lakini wapinzani walikuwa nyuma muda wote ikawa changamoto kuwafungua ingawa tulipata bao moja.

Kiungo huyo wetu wa zamani ameongeza kuwa kipindi cha pili City walivyo funguka kuja kutushambulia tukapata nafasi ya kuwafunga mabao mawili.

Advertisement

"Kwanza tunamshukuru Mungu kwa ushindi huu pili nawapongeza wachezaji kwa kujituma kufanikisha tunapata alama tatu muhimu katika uwanja wa nyumbani.

"Kipindi cha kwanza wapinzani walikuwa nyuma wote kuzuia walipofunguka cha pili tukawafunga mawili," amesema Matola.

Back to homepage
Share this story