Simba Sports Club
News

Mashabiki wamwagia pesa Wawa wakimuaga

23 Jun 2022

Mchezo wa leo ni wa mwisho kwa Wawa kucheza ndani ya kikosi chetu baada ya kudumu kwa miaka mitano na ulipangwa rasmi kumuaga nyota huyo wa kimataifa kutoka Ivory Coast.

Mashabiki wetu wameonyesha upendo mkubwa kwa Wawa kama ilivyokuwa kwa kiungo mshambuliaji Rally Bwalya ambaye naye alitunzwa pesa.

Advertisement

Tumeweka utaratibu mzuri kwa kuhakikisha tunamalizana vizuri na wachezaji wetu kwa kuwaaga mbele ya mashabiki wetu kutokana na kuthamini michango yao ndani ya klabu yetu.

Back to homepage
Share this story